UVUVI

UVUVI HARAMU WAZIDI KUHATARISHA MAISHA YA MAMA WAJAWAZITO
TOA MAONI JINA NA MAHALI
Athari ya uvuvi haramu ambazo zimekua zikitajwa kwa watu wanaokula samaki wanaovuliwa na sumu zimeanza kujitokeza na iwapo hatua ya kutokomeza ujangiri huu hazitachukuliwa haraka kuna uwezekano wa watumiaji kupata madhara zaidi ya kiafya.
Baadhi ya athari hizo ni mimba za wanawake kutoka au kuzaa watoto wenye mapungufu, kupoteza nguvu za kiume na za kike pamoja na kupata ugonjwa wa kansa.
Samaki ni Kitoweo kilichokua na faida nyingi mwilini mojawapo ni kuwa na mafuta yenye kiambata aina ya Omega 3 yanayomfanya binadamu kuwa na uwezo mkubwa wa kufikiri, kutunza kumbukumbu na kuishi kwa muda mrefu.
Uvuvi haramu umebadilisha yote hayo.

January hadi february mwaka huu wanawake 55 mimba zao ziliharibika lakini hakuna uthibitisho wa moja kwa moja kama ni sumu ya samaki.
Mara nyingi imekua vigumu kwa mlaji kubaini samaki aliyevuliwa kwa sumu lakini baadhi ya wafanyabiashara wa samaki wanadai kuwatambua.
Feb 30 mwaka huu katika kijiji cha Bukondo majira ya saa 7 usiku wavuvi haramu 11 wamekamatwa wakiwa na makokoro ya dagaa chini ya mililita 8 ambayo yanauwezo wa kuvua sangara na sato na wengi wao ni vijana wanaotumiwa kufanya shughuli hizi.

No comments:

Post a Comment